Our Feeds
#htmlcaption1

Wednesday, June 14, 2017

habarimoto255

MAMISA NI MZAZI MWENZANGU TU HAKUNA CHA ZIADA - YOUNG DEE

Msanii wa Bongo Fleva na hit maker wa winbo ‘Bongo Bahati Mbaya’ ameendelea kusistiza kuwa hakuwahi kuwa na mahusiano ya kimapenzi na mzazi mwenzie ‘Mamisa’.


Rapper huyo amekiambia kipindi cha 5 Selekt cha EATV kuwa kilichotokea hakikuwa katika mipango yake hivyo sasa hivi kila mmoja ana maisha yake.

“Am single and am buys, sina mahusiano, ni kitu ambacho naweza kusema kibinadamu kinatokea kama baraka tu kwa sababu hakuwahi kuwa mpenzi wangu, imebaki kama ilivyokuwa mwanzoni.” amesema Young Dee.

Katika hatua nyingine amezungumzia mafanikio aliyoyapata hadi sasa kupitia wimbo wa Bongo Bahati Mbaya.“Kikubwa imedhihirisha kuwa watu bado wanapenda muziki mzuri, watu bado wanapenda muziki wa hip hop.

Kwangu mimi ni kitu ambacho kimenipa faraja na nguvu ya kuendelea kufanya kazi nzuri,” ameeleza Young Dee.

Subscribe to this Blog via Email :
Previous
Next Post »